Sinopsis
Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.
Episodios
-
Kenya: Yawarejesha nyumbani raia wake waliotapeliwa kuenda Mynamar
08/04/2025 Duración: 09minShaba yetu kwenye makala haya inalenga hatua ya Serikali ya Kenya, kueeendelea kuwarejesha mamia ya raia wake waliotapeliwa na kusafirishwa hadi nchini Myanmar kwa ahadi ya kupewa ajira. Nchini mwako visa kama hivi vinaripotiwa?Ndilo swali letu, skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.
-
Africa Mashariki : Viongozi watathimini kudhibiti mitandao ya kijamii
08/04/2025 Duración: 09minKatika makala haya tunajadili haja ya kuwepo sheria za kudhibiti mitandao ya kijamii kwa baadhi ya mataifa ya Africa Mashariki. Skiza makala haya kuskia mano ya waskilizaji wetu.
-
Maoni ya waskilizaji kuhusu wizi unaofanywa kwenye mizani na wafanyabiashara
05/04/2025 Duración: 10minMakala haya ni maoni ya waskilizaji kuhusu ripoti maalum ya namna wananchi wanavyopigwa na wafanyabiashara kwenye mizani wanapopimiwa nafaka mbalimbali za chakula, huku gesi ya kupikia pia ikitajwa.
-
-
DRC: Majadiliano ya kitaifa kuhusu kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa kitaifa
25/03/2025 Duración: 10min -
Qatar : Yakutanisha Kagame na Tshisekedi
20/03/2025 Duración: 09minShaba yetu leo kwenye makala haya inalenga taifa la Qatar ambapo taifa hilo juma hili lilifanikiwa kuwaleta pamoja marais Felix Tshiesekedi wa DRC na mwenzake wa Rwanda Paul Kagme, katika juhudi za kutafuta suluhu kwa mzozo wa mashariki ya DRC. Unafikiri Qatar itafanikiwa kuzima mzozo wa mashariki mwa DRC. Skiza makala haya kujua baadhi ya maoni ya waskilizaji.
-
Kenya : Kanisa katoliki latangaza marufuku kwa wanasiasa
19/03/2025 Duración: 10minTunajadili hatua ya Kanisa la Anglikana nchini Kenya, kwa mara nyingine limesisitiza marufuku ya kuwazuia wanasiasa kuzungumza kanisani katika juhudi za kuzuia wanasiasa kufanya siasa kanisani. Je unazungumziaje hatua hii ya kanisa Anglikana nchini Kenya? Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu.
-
Rwanda yasitisha uhusiano na Ubelgiji
18/03/2025 Duración: 09minKatika makala haya tunajadili hatua ya serikali ya Rwanda, kutangaza kusitisha uhusiano wa Kidiplomasia na taifa la Ubelgiji kutokana na kile Rwanda imesema Ubelgiji kuendeleza propaganda kuihusu kutokana na mzozo wa mashariki mwa DRC. Unazungumziaje hatua ya Rwanda Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.
-
Watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi
17/03/2025 Duración: 10minTunajadili hatua ya bazara la wakikimbizi la Denmark, kuchachapisha ripoti inayoonesha kuwa, watu zaidi ya milioni 6 duniani watakosa mahali pakuishi ifikapo mwishoni mwa mwaka ujao, kutokana na mizozo, mabadiliko ya tabia nchi na kusitishwa kwa misaada toka Marekani. Unazungumziaje hatua hii? ndilo swali tumeuliza, skiza makala haya kufahamu mengi.
-
Maoni yako kutokana na habari zetu juma hili
14/03/2025 Duración: 10minKila Ijumaa rfi Kiswahili inatoa nafasi kwa mskilizaji kuchaniua mada mbalimbali kuhusu taarifa zetu. Juma hili hizi ni haya ni baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu
-
DRC : Angola kufanikisha mkutano kati ya rais Tshisekedi na waasi wa M23
13/03/2025 Duración: 09minShaba yetu inalenga nchini DRC, ambapo taifa la Angola limesema linajaribu kufanikisha mazungumzo ya moja kwa moja kati ya rais wa DRC, Felix Tshisekedi na waasi wa M23, ili kutafuta suluhu la mzozo wa mashariki mwa DRC. Je unafiriki Angola itafanikiwa katika hili?Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Sudan Kusini :Wanajeshi wa Uganda wawasili Sudan Kusini
13/03/2025 Duración: 09minMkuu wa majeshi nchini Uganda, ambaye pia ni mwana wa rais Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba, amedai wanjeshi wa taifa lake wamewasili Sudan Kusini ili kusaidia jeshi la taifa hilo kutatua mzozo ndani ya serikali ya umoja wa kitaifa Tunakuuliza je mzozo wa Sudan Kusini unastahili kutatuliwa kijeshi?Skiza makala haya kuskiza baadhi ya maoni yenu.
-
Kenya: Vijana wapinga michango ya wanasiasa kanisani
11/03/2025 Duración: 09minShaba yetu leoinalenga nchini Kenya ambapo Vijana wameanza kuandamana kupinga kile wanadai wanasiasa kutoa kiasi kikubwa cha pesa kwenye maeneo ya kuabudu ili hali wao hawana ajira. Tumekuuliza hatua hii ni sahihi?Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Kenya : Rais Ruto na mpinzani Raila Odinga kushirikiana
11/03/2025 Duración: 09minMwishoni mwa juma lililopita rais wa Kenya William Ruto na kiongozi wa upinzani Raila Odinga walitiliana saini mkataba wa ushirikiano wa kisiasa, wanaosema utasaidia kutatua changamoto zinazowakabili raia wa taifa hilo. Unaamini makubaliano ya viongozi hawa ni sahihi?Ndilo swali tumekuuliza na haya hapa maoni yako.
-
Hatua ya rais Donald Trump kusitisha msaada wakijeshi kwa nchi ya Ukraine
06/03/2025 Duración: 10min -
Maoni kuhusu vingozi wa kijeshi wa nchi za Afrika Magharibi kutaka kugombea urais
05/03/2025 Duración: 10minNchini Gabon, kiongozi wa kijeshi jenerali Brice Oligui Nguema ametangaza kuwa atagombea urais katika uchaguzi wa mwezi ujao, baada ya kutwaa madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi ya 2023.Hili linajiri wakati huu viongozi wengine wa kijeshi kwenye nchi za Burkina Faso, Mali na Niger wakielekea kuchukua mkondo huo.
-
-
Kila Ijumaa ni mada huru ambapo unatoa maoni kuhusu ulichokiona wiki hii
28/02/2025 Duración: 10minLeo ni Ijumaa ,,siku ya mada huru kwenye habari rafiki ambapo Tunakupa nafasi ya kuzungumzia suala lolote ambalo limetokea nchini mwako wiki hii au kile ambacho umekisikia kwenye matangazo yetu ya juma hili
-
Rais wa Uganda Yoweri Museveni asikitishwa na hali ya umaskini nchini mwake
27/02/2025 Duración: 10minMada ni kuhusu..kauli ya Rais wa Uganda Yoweri Museveni Akiwa katika ziara ya kawaida kuzungumza na raia wake , ameeleza kuguswa na kusikitishwa na hali ya umasikini anayoshuhudia kwenye nchi yake,,,wakati huu tatizo la umasikini linashuhudiwa pia kwenye mataifa mengine ya ukanda.Tulimuuliza mskilizaji anazungumziaje kauli ya Rais Museveni na je viongozi wa ukanda wamefanya vyakutosha kupambana na umasikini?
-
Rais wa DRC, Felix Tschsekedi, atangaza kuunda Serikali ya umoja wa kitaifa
24/02/2025 Duración: 10minKaribu kwenye kipindi cha leo ambapo tunaangazia tangazo la Rais wa DRC, Felix Tschsekedi, kuwa ataunda Serikali ya umoja wa kitaifa, hatua inayokuja wakati huu akiwa katika shinikizo kutoka ndani na nje ya nchi yake, kuhusu namna alivyoshughulikia mzozo wa mashariki mwa nchi yake, wakati huu waasi wa M23 wakichukua miji zaidi.