Habari Rfi-ki

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:59:17
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

Episodios

  • Marais wa Afrika kusalia madarakani kwa muda mrefu hata umri ukiwa umeenda

    15/07/2025 Duración: 09min
  • Viongozi wa Afrika watuhumiwa kuahidi mengi na kutimiza machache

    15/07/2025 Duración: 09min
  • Kila Ijuma unapata nafasi kuchangia chochote ndani ya rfi Kiswahili

    15/07/2025 Duración: 09min

    Kila Ijumaa rfi kiswahili inakupa nafasi ya kuchangia mada yoyote ile kwenye makala haya. Skiza maoni ya waskilizaji.

  • Kenya : Maandamano yatumika kupora mali

    15/07/2025 Duración: 09min

     Maandamano nchini Kenya na mataifa  mengine ya Afrika  yamekumbwa na mauaji na uporaji huku mali za watu zikiharibiwa. Je, unafikiri ni sahihi kwa waandamanaji kupora na kuharibu mali za watu? Nini vyombo vya usalama vinapaswa kufanya kuzuia uharibifu? Haya hapa baadhi ya maoni yako.

  • Viongozi wa Afrika wanatuhumiwa kuahidi mengi wakati wa kampeni na kutotimiza

    14/07/2025 Duración: 09min
  • Kenya: Mahakama ya juu yasema mwana haramu si haramu

    09/07/2025 Duración: 09min

    Katika makala haya tujadili hatua ya mahakama ya juu zaidi nchini Kenya, kuagiza kwamba mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa kwenye dini ya kiislamu ana haki ya kumiliki mali ya babake kama watoto wengine waliozailiwa ndani ya ndoa, hatua inayoenda kinyume kabisa na tamaduni za dini hiyo. Unazungumziaje uamuzi huu wa mahakama nchini Kenya ? Haya hapa baadhi ya maoni yako.

  • Côte d'Ivoire : Kurejeshewa ngoma maalum kutoka Ufaransa

    08/07/2025 Duración: 09min

    Kaika makala haya tunajadili  hatua ya bunge nchini Ufaransa kupiga kura na kupitisha mswada wa kurudishwa nchini Ivory Coast ngoma maalum inayozungumza iliyochukuliwa katika nchi hiyo ya Afrika kutoka kabila la Ebrie wakati wa ukoloni mwaka 1916. Je umefika wakati kwa koloni za zamani za Bara la Afrika kurejesha vyombo walivyopora ?   Ndilo swali tumekuuliza . Haya hapa maoni yako.

  • Siku ya lugha ya kiswahili duniani makala maalum

    07/07/2025 Duración: 10min

    Siku ya kiswahili duniani, ambayo imekuwa ikiadhimishwa tangu mwaka 2022. Maadhimisho ya mwaka huu imefanyika jijini Kigali nchini Rwanda, ambako mamia ya wataalam na wapenzi wa Kiswahili wamekutana kwa siku mbili kujadiliana kuhusu nafasi na umuhimu wa lugha ya Kiswahili kwa raia wa nchi zote za Jumuiya. Kauli mbiu ni kusherehekea lugha ya Umoja, utambulisho na mchango wake kwa dunia.RFI kiswahili imeshirikiana na taasisi ya mafunzo ya biashara na ufundi stadi, NIBS ya jijini Nairobi, kuandaa makala maalum ya Habari RAFIKI na mwandishi wetu Ruben Lukumbuka ameongoza makala hii

  • Maoni yako kwenye mada huru Ijumaa hii

    04/07/2025 Duración: 09min
  • Watu karibu 500 wakamatwa nchini Kenya kufuatia maandamano ya Juni 25 2025

    02/07/2025 Duración: 10min

    Wanatuhumiwa kwa mauaji, ugaidi, ubakaji na makosa mengine. Wanaharakati wa haki za binadamu, wanasema, wanawake 14 walibakwa wakati wa maandamano hayo.

  • Maoni yako kuhusu azma ya rais wa Uganda Museveni kuwania tena urais

    01/07/2025 Duración: 09min
  • Mkataba kati ya DRC na Rwanda ya kuleta amani yakudumu mashariki mwa DRC

    30/06/2025 Duración: 09min

    Umoja wa Afrika umekaribisha makubaliano yaliyotiwa saini mwishoni mwa juma lililopita kati ya Rwanda na DRC, hatua ambayo itashuhudia unyang'anyaji wa silaha na kuondolewa kwa mamluki wa kigeni mashariki mwa Congo.

  • Matukio ya wiki likiwemo kuelekea kusainiwa mkataba wa amani nchini DRC

    27/06/2025 Duración: 10min
  • Hatua ya bunge la Uingereza kuruhusu huduma ya kusaidiwa kufa

    26/06/2025 Duración: 09min

    Bunge la Uingereza hivi majuzi liliidhinisha mswada wa huduma ya kusaidiwa kufa

  • Maandamano ya kumbukizi ya kuwauwa kwa vijana zaidi ya 60 mwaka jana

    25/06/2025 Duración: 10min

    Waandamanaji wakabiliana na polisi siku nzima wakati ya maandamano ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha wakati wa maandamano ya mwaka jana ya Gen Z

  • Zambia :Rais Hakainde Hichilema asisitiza serikali kufanya mazizi ya Edgar Lungu

    24/06/2025 Duración: 10min

    Rais wa Zambia Hakainde Hichilema ameendelea kusisitiza kufanya mazishi ya kitaifa kwa mtagulizi wake Edgar Lungu Licha ya mzozo uliopo baina yake na familia juu ya utekelezwaji ya matakwa ya marehemu ya kukataa kufanyiwa mazishi ya kitaifa.Tunakuuliza maoni yako kuhusu mzozo huo.

  • MAONI: DRC na Rwanda zitie saini makubaliano kumaliza mauaji ya raia

    20/06/2025 Duración: 10min

    Kila siku ya Ijumaa, hapa RFI Kiswahili, tunampa mskilizaji wetu nafasi kuzungumzia habari kuu ambazo tumekuwa nazo wiki hii au kutueleza jambo lolote ambalo limetokea nchini mwake. Wiki hii maoni mseto yameangazia, miongoni mwa taarifa zingine, tangazo kwamba Rwanda itatia saini makubaliano na DRC tarehe 27 Juni, kumaliza mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, lakini pia mashambulio baina ya Israeli na Iran.

  • Burundi : Rais Ndayishimiye ataka mazungumzo na upinzani

    16/06/2025 Duración: 10min

    Rais wa Burundi Evariste #Ndayishimiye ametoa wito kwa upinzani kushiriki katika mazungumzo na chama chake CNDD-FDD baada ya uchaguzi wa wiki iliyopita ambao ulikumbwa na upinzani mkubwa kwa ukosefu wa uwazi.   Hata hivyo upinzani haujaonyesha nia ya kushiriki mazungumzo hayo. Tunakuuliza, ni sahihi upinzani kujiunga na serikali ? skiza makala haya kuskia maoni ya mskilizaji.

  • Utumwa wa watoto waendelea kuripotiwa licha ya juhudi mbalimbali zinazowekwa

    13/06/2025 Duración: 09min

    Juni 12, ni Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ajira kwa Watoto. Inakadriwa, takriban watoto milioni 200 kote duniani wanatumikishwa badala ya kuwa shuleni.   Tunakuuliza, serikali yako inafanya vya kutosha kukomesha utumwa wa watoto? Unamfahamu mtoto anayefanyishwa kazi?

  • Kwa nini wanaume wanashindwa kutafuta ushauri wa afya ya akili

    13/06/2025 Duración: 10min

    Makala haya yanaangazia afya ya akili, ikizingatiwa kuwa Juni ni Mwezi wa Uhamasishaji wa Afya ya Akili ya Wanaume.   Unafikiri ni kwanini wanaume wanashindwa kutafuta ushauri wa afya ya akili? Unadhani afya ya akili ya mwanaume inasahaulika? Skiliza makala ya leo usikie maoni kutoka kwa waskilizaji wetu.

página 1 de 2