Sbs Swahili - Sbs Swahili

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 128:06:52
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.

Episodios

  • Taarifa ya habari tarehe 21 Novemba

    21/11/2025 Duración: 11min

    Elekea kwenye tovuti yetu katika sbs.com.au/swahili kwa habari na taarifa zaidi.

  • Taarifa ya habari tarehe 18 Novemba

    21/11/2025 Duración: 10min

    Elekea kwenye tovuti yetu katika sbs.com.au/swahili kwa habari na taarifa zaidi.

  • Taarifa ya habari tarehe 14 Novemba

    21/11/2025 Duración: 10min

    Elekea kwenye tovuti yetu katika sbs.com.au/swahili kwa habari na taarifa zaidi.

  • Taarifa ya habari tarehe 11 Novemba

    21/11/2025 Duración: 12min

    Elekea kwenye tovuti yetu katika sbs.com.au/swahili kwa habari na taarifa zaidi.

  • Yaliyojiri Afrika 21 Novemba

    21/11/2025 Duración: 08min

    Jason Nyakundi anatujuza yaliyojiri Afrika

  • Yaliyojiri Afrika 18 Novemba

    21/11/2025 Duración: 08min

    Jason Nyakundi anatujuza yaliyojiri Afrika

  • Yaliyojiri Afrika 14 Novemba

    21/11/2025 Duración: 06min

    Jason Nyakundi anatujuza yaliyojiri Afrika

  • Yaliyojiri Afrika 11 Novemba

    21/11/2025 Duración: 06min

    Jason Nyakundi anatujuza yaliyojiri Afrika

  • Yaliyojiri Afrika 7 novemba

    21/11/2025 Duración: 07min

    Jason Nyakundi anatujuza yanayojiri Afrika.

  • Tahadhari kwa wanaohitimu shule

    21/11/2025 Duración: 04min

    Kadri maelfu ya vijana wanaposherehekea kumaliza Mwaka wa 12, wanakumbushwa juu ya hatari zinazokuja na unywaji pombe, hasa nje ya nchi. Wazazi na marafiki wa waathiriwa wa sumu ya methanol, Bianca Jones na Holly Bowles, wamejiunga na juhudi mpya za usalama, wakiwatia moyo wasafiri vijana kuchukua maamuzi salama zaidi.

  • Programu za kufunza watu wazima kusoma na kuandika

    21/11/2025 Duración: 05min

    Mmoja kati ya Waaustralia watano, au takriban watu wazima milioni tatu, wana kiwango cha chini cha ujuzi wa kusoma na kuandika au hesabu - na hii inaweza kuwa na athari kubwa katika jinsi watu wanavyoweza kushiriki maisha ya kila siku. Programu zimewekwa kote nchini kusaidia watu kuboresha ujuzi wao na kufikia malengo yao ya maisha. Ikiwemo moja huko Tasmania, ikiwasaidia watu wazima kuwa tayari kwa kazi.

  • Watu wa asili kwenye hatihati ya kutoweka Brazil

    18/11/2025 Duración: 08min

    Shirika lisilo la faida linasema karibu nusu ya jamii za Wenyeji wanaoishi mbali na ulimwengu wanakabiliwa na kutoweka ndani ya muongo kutokana na ukataji miti, uchimbaji wa madini na utalii. Survival International wanasema wanataka ulimwengu - hususan serikali na viwanda - kutambua na kushughulikia tatizo hili kama dharura ya kimataifa.

  • Uzalishaji wa Net Zero nchini Australia

    18/11/2025 Duración: 08min

    Muungano umeidhinisha rasmi kuondoa lengo la kutofikia uzalishaji wa gesi chafu katika mkutano wa chumba cha chama huko Canberra. Zaidi ya hayo, Liberals na Nationals wamefunua mpango wa kuondoa mabadiliko ya tabianchi kutoka kwenye orodha ya malengo ya mdhibiti wa nishati ya kitaifa, huku wakiapa kuendelea kupunguza uzalishaji kwa kufuatilia maendeleo ya nchi nyingine.

  • Maumivu ya wanawake kutiliwa maanani zaidi

    14/11/2025 Duración: 08min

    Serikali ya Victoria imetoa ripoti ya mwisho ya uchunguzi kuhusiana na uzoefu wa wanawake katika suala la maumivu - na ni taarifa inayosumbua kusoma. kutokana na uzoefu wa wanawake na wasichana 13,000, ripoti hiyo imebaini mapengo katika huduma za afya kwa jinsia, upendeleo katika matibabu, ubaguzi wa kijinsia, na hisia za kupuuzwa au kutopingwa na wataalamu wa afya zinazoenea katika mfumo wa afya wa Victoria.

  • Maandamano ya kikundi cha NSN uliwezaje kuruhusiwa kufanyika

    14/11/2025 Duración: 08min

    Maandamano ya neo-Nazi mbele ya bunge la New South Wales yamezua mshtuko katika jamii za Kiyahudi na za tamaduni mbalimbali huko Sydney. Serikali ya jimbo hilo imekashifiwa baada ya kufichuliwa kwamba tukio hilo liliendelea na idhini kutoka kwa Polisi wa New South Wales. Je, ni vipi maandamano haya ya neo-Nazi yalipewa kibali cha kufanyika mwanzoni?

  • Mazungumzo kuhusu African Youth Summit 2025

    14/11/2025 Duración: 11min

    Mkutano wa kwanza wa African Youth Summit uliandaliwa na kufanyika mwaka huu, na mratibu wa vijana aliyehudhuria anajiunga nasi kuzungumzia mada ya mkutano huo.

  • Idadi ya watoto wa mataifa ya kwanza gerezani yazua tashwishi

    11/11/2025 Duración: 08min

    Serikali ya majimbo na maeneo nchini Australia zitachunguzwa kama sehemu ya uchunguzi wa bunge kuhusu matokeo na athari za kifungo kwa vijana. Kati ya maswala ya kuzingatia katika uchunguzi huu ni Kuzidishwa kwa kufungwa kwa watoto wa Mataifa ya Kwanza.

  • Serikali kudhibiti mitandao ya kijamii kuanzia desemba

    11/11/2025 Duración: 06min

    Mtandao wa Reddit na jukwaa la Kick zitaongezwa kwenye majukwaa yanayohitajika kuzuia watumiaji walio na umri chini ya miaka 16, sheria mpya zitakapoanza kutekelezwa mwezi Desemba. Marufuku ya Australia ya mitandao ya kijamii kwa watoto chini ya miaka 16, ambayo inajumuisha majukwaa nane kuu, inategemea tathmini zinazoendelea za eSafety ambazo zinaweza kufafanua kati ya huduma za mitandao ya kijamii, ujumbe, na michezo, kuelezea ni kwanini majukwaa kama Steam na Twitch hayakujumuishwa. Wakati serikali ilihakikishiwa na Roblox kwamba wataanzisha teknolojia za kuthibitisha umri ili kupunguza tabia za uwindaji wa watoto, watetezi wa haki za kidigitali wanatahadharisha kwamba marufuku haya yanaweza kuhamasisha watoto kutumia majukwaa madogo yasiyo na uangalizi ambapo wanaweza kukumbana na madhara makubwa zaidi.

  • Viza ya milioni moja kutolewa nchini Australia

    11/11/2025 Duración: 07min

    Australia inatarajia kutoa kibali cha kila kudumu ama permanent humanitarian visa , cha milioni moja tangu kumalizika kwa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwisho wa mwaka huu. Hatua hii imewezesha sherehe juu ya mchango mkubwa ambao wakimbizi hufanya katika hadithi ya kitaifa ya Australia. Lakini mashirika ya haki za wakimbizi yanasema ni wakati muafaka kufikiria jinsi Australia inaweza kuboresha jibu lake kwa ukimbizi mkubwa wa dunia nzima.

  • Mfumo wa utoaji wa mayai ya uzazi Australia huenda ukabadilika

    11/11/2025 Duración: 08min

    Mahitaji ya mayai ya uzazi yanaongezeka nchini Australia kadiri watu wanavyokumbwa na changamoto za uzazi. Lakini mahitaji ya mayai ni makubwa mno kuliko upatikanaji wao na sasa, wataalamu wanapendekeza Australia ifikirie kubadilisha kanuni zinazohusu utoaji mayai.

página 1 de 32