Sinopsis
Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Episodios
-
Amnesty International : Saudi Arabia inawanyanyasa wafanyakazi wa nyumbani
23/05/2025 Duración: 09minShirika la Amnesty International imeitaka serikali ya Kenya pamoja na ile ya Saudi Arabia kushiriiana na kuweka mikakati ya kuhakikisha haki za raia wa Kenya wanaofanya kazi katika mataifa ya Ugaibini hazitatiziki. Katika ripot iyake Amnesty imesema kuwa wanawake wanaofanya kazi za nyumbani huko Uarabuni wanapitia mateso za kijinsia, kunyanyashwa kimapato na hata kuuawa.
-
Kenya : Demokrasia inavyotafsiriwa Africa
18/05/2025 Duración: 09minKatika makala haya tunazama kuangazia swala zima la demokrasia na uhusiano wake na haki za binadamu.Unavyofahamu mskilizaji demokrasia mara nyingi hotofautiana na mazingira ya nchini mbalimbali duniani. Mara kadhaa swala demokrasia limehusishwa na haki za binadamu, katika makala haya Benson Wakoli anajadili swala hili na muasisi wa shirika la utafito la Afro barometer Jane Wanga ambaye pia ni mhadhiri katika chuo kikuu cha Nairobi kufahamu uhuasiano uliopo kati ta demokrasia na haki za binadamu.
-
Afrika Mashariki : Sikuku ya leba ina maana gani kwa wafanyakazi
06/05/2025 Duración: 09minWafanyakazi ndio wanainua majengo, kufundisha watoto, kuwahudumia wagonjwa, kuendesha uchumi wa Afrika Mashariki. Lakini je, haki za wafanyakazi kazini zinalindwa ? kila mwaka Mei mosi dunia huadimisha siku ya kimataifa ya wafanyakazi — na kwenye makala haya, tunaangazia kilio na matumaini ya wafanyakazi wa Afrika Mashariki wanaopigania haki zao za msingi kazini.Muungano wa kimataifa wa wafanyakazi — ILO — linatambua haki kadhaa muhimu kwa kila mfanyakazi moja ni :Haki ya kupata mshahara wa heshimaHaki ya kufanya kazi kwa saa zinazokubalikaHaki ya kujiunga na vyamaHaki ya usalama kaziniHaki ya kutobaguliwaSkiza makala haya kufahamu mengi zaidi.
-
Tanzania: Haki ya kusikiliza kesi mahakamani
30/04/2025 Duración: 10minNchini Tanzania, wafuasi na wanasiasa wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, walikamatwa na kupigwa na maafisa wa polisi walipokwenda Mahakamani jijini Dar es salaam, kusikiliza kesi ya uhaini na uchochezi inayomkabili kiongozi mkuu wa upinzani CHADEMA, Tundu Lissu.Katika makala ya leo ya Jua Haki yao, tunaangazia Uhuru wa kufauta kesi mahakamani, kwanini kuna haki ya kusikiliza kesi mahakamani na kwa nini mataifa mengi barani afrika yanazuia raia kusikiliza kesi kama hizi mahakamani.