Jua Haki Zako

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 3:48:21
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.

Episodios

  • Kenya: Uhuru wa kutumia mitandao ya kijamii na mipaka yake

    09/01/2025 Duración: 10min

    Siku ya Jumatatu asubuhi Vijana wanne kati ya 6 waliotekwa nyara katika wiki za hivi majuzi waliachiliwa huru, saa chache kabla ya maandamano yaliyopangwa kufanyika kupinga kutoweka kwao.  Billy Munyiri Mwangi na Peter Muteti waliungana na familia zao huko Embu na Nairobi, mtawalia, baada ya kuzuiliwa kwa zaidi ya wiki mbili ilhali Rony Kiplangat alipatikana katika kaunti ya Machakos naye Benard Kavuli akapatikana katika maeneo ya Kitale magaribi mwa nchi. Katika makala Jua haki zako, tunaangazia huru wa kutumia mitandao ya kijamii na katika kutumia mitaoa hiyo kuna mipaka yake. Je nchini Kenya hatua zipi zinafaa kuchukuliwa ikiwa mshukiwa atapatikana na hatia ya kukiuka huru ywa mitandao ya kijamii.

  • Dunia:Haki za wanawake na Ukomeshaji wa visa vya mauaji

    30/12/2024 Duración: 09min

    Makala jua haki zako leo yataangazia haki za kina dada,changamoto wanazopitia na nini wanaharakati wanafanya ili kuhakikisha visa vya dhulma vinaripotiwa kwa wakati na haki inatendeka.Kumbuka killa mwaka, kuanzia tarehe 25 Novemba hadi 10 Disemba, dunia inaungana kwa pamoja kutambua changamoto kubwa zinazowakumba wanawake na wasichana, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia, ukatili wa kifamilia, na vitendo vingine vyote vya ubaguzi na dhuluma.

  • Kenya : Akili dada na Juhudi zake za kuinua maisha ya mtoto wa kike

    18/12/2024 Duración: 10min

    Joy Zawadi, mkurugezi mkuu wa shirika la Akili Dada, linalopigania haki za mtoto wa kike alikiti chini na Benson Wakoli, kujadili juhudi wanazofanya kuinua mtoto wa kike nchini Kenya. Kufahamu mengi zaidi skiza makala haya.

página 2 de 2