Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
Ripoti: Matajiri wachache wanateka nyara dunia kwa kuchangia pakubwa utoaji wa hewa ukaa
- Autor: Vários
- Narrador: Vários
- Editor: Podcast
- Duración: 0:09:58
- Mas informaciones
Informações:
Sinopsis
Dunia inapojiandaa kwa mkutano wa kimataifa wa Mazingira COP30 utakaofanyika Belém, Brazil, ripoti mpya imeibua mjadala mkali—si tu kuhusu uzalishaji wa hewa ukaa, bali pia kuhusu ukosefu wa usawa. Utafiti mpya wa shirika la Oxfam, unaonesha kuwa mataifa tajiri na watu wachache wenye utajiri mkubwa wanachangia kwa kiasi kikubwa katika mabadiliko ya tabianchi. Inaitwa “ukosefu wa haki wa hali ya hewa.” Mtaalam wetu leo kulichambua hili ni David Abudho, anayeshughulika na mabadiliko ya tabia nchi barani Afrika kutoka shirika la Oxfam.