Sinopsis
Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.
Episodios
-
Mkutano wa Luanda kati ya DRC na waasi wa M23 marchi 18, hali ya sudani na kwengineko
15/03/2025 Duración: 20minMazungumzo ya ana kwa ana kati ya DRC na waasi wa M23 wanaosaidiwa na Rwanda kuanza jumanne ya Marchi 18, SADC kusitisha operesheni zake mashariki mwa DRC, mapigano kule Sudan Kusini kati ya wanajeshi wa serikali na wapiganaji waliotiifu kwa makamu wa kwanza wa rais Riek Machar, juhudi za kikanda kuyahamasisha mataifa ya Mali, Burkina faso na Niger kurejea tena kama wanachama wa ECOWAS, na sitisho la mapigano kwa muda mfupi kati ya Urusi na Ukraine, ni miongoni mwa yaliyojiri wiki hii
-
Muungano wa Rais wa Kenya W. Ruto na Raila Odinga, hali mbaya ya kibinadamu DRC
08/03/2025 Duración: 20minRais wa Kenya William Ruto na aliyekuwa kiongozi wa upinzani Raila Odinga wameungana kisiasa rasmi, hali ya mzozo wa mashariki mwa DRC Kuchukua sura mpya, vikwazo vya kiuchumi kuikumba nchi ya Rwanda kufuatia uungwaji mkono wake kwa kundi la waasi la M23, Kiongozi wa kijeshi wa Gabon jenerali Oligui Nguema kuwania urais mwezi ujao, mzozo wa kibiashara kati ya Marekani nchi mataifa kadhaa, lakini pia mzozo wa Ukraine na Urusi.
-
Rais Donald Trump na Volodymyr Zelensky watofautiana kuhusu vita nchini Ukraine
04/03/2025 Duración: 19minWiki hii kwenye habari za ulimwengu tunaangalia majibizano makali kati ya rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Ukraine Volodymyr Zelensky katika Ikulu ya White House, pia tunaangalia mikakati inayowekwa kumaliza mgogoro wa DRC huku Rwanda ikisema haitishwi kutengwa na ulimwengu, Somalia na Ethiopia zarejesha uhusiano wa kidiplomasia, mkutano wa G20 ukikamilika kule Afrika Kusini bila mwafaka kufikiwa.
-
Kizza Besigye wa Uganda ashtakiwa kwa uhaini, Kenya na Sudan zatofautiana kuhusu RSF
23/02/2025 Duración: 19minHabari za wiki hii ni pamoja na hali kule nchini Mashariki mwa DRC, utata wa kidplomasia uanozingira Kenya na Sudan, tutaangazia pia kesi ya kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye, lakini tutaangalia kipindi cha mpito nchini Niger. Tumedadisi pia hali kufikia sasa ya vita vya kule Gaza na misimamo ya viongozi mbalimbali wa ulimwengu.