Mtazamo Wako Kwa Yaliyojiri Wiki Hii

  • Autor: Vários
  • Narrador: Vários
  • Editor: Podcast
  • Duración: 8:03:11
  • Mas informaciones

Informações:

Sinopsis

Makala yanayochambua masuala na matukio mbalimbali yaliyotokea kwenye jamii kwa wiki nzima kwa kina, yanatoa fursa kwa msikilizaji kueleza hisia na mtazamo wake juu ya masuala yanayoendelea kutokea iwe ni katika uga wa uchumi na siasa duniani kote.

Episodios

  • Israeli na wapiganaji wa Hamas wakubaliana kusitisha vita huko Gaza

    18/01/2025 Duración: 20min

    Miongoni mwa yale tumekuandalia wiki hii ni pamoja na kuapishwa kwa Rais Mteule wa Marekani Donald Trump, mapigano yanyoendelea kuripotiwa mashariki ya DRC, makubaliano ya kusitishwa kwa vita kati ya Hamas na Israeli.

  • Mapigano mashariki mwa DRC, ziara ya rais Ruto nchini Angola na mengineyo

    11/01/2025 Duración: 20min

    Makala hii imeangazia mapigano eneo la mashariki mwa DRC, mvutano wa kisiasa nchini Kenya pamoja na hali ya Sudan, kauli ya rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwamba mataifa ya Afrika hayana shukrani katika kuyataka majeshi ya Ufaransa kuondoka kwenye ardhi zao na mazishi ya aliyekuwa rais wa 39 wa Marekani Jimmy Carter wiki hii

  • Mwaka mpya wa 2025 na matarajio ya ulimwengu kuhusu usalama amani na maendeleo

    04/01/2025 Duración: 20min

    Makala hii imeangazia namna ambavyo nchi zetu zilivyoukaribisha mwaka wa 2025 kwa shamrashamra za kila aina huku wakisema kwaheri kwa mwaka 2024 ulioshuhudia michezo mikubwa zaidi ulimwenguni ya Olimpiki, vita ya Ukraine na kule Gaza, usalama mashariki mwa DRC, Sudan pamoja na kurejea madarakani kwa aliyekuwa rais wa Marekani, Donald Trump.

  • Polisi wa Kenya wasambaratisha maandamano, hotuba ya Tshisekedi bungeni DRC

    14/12/2024 Duración: 20min

    Makala imeangazia namna ambavyo polisi nchini Kenya walivyotawanya maandamano ya wanaharakati waliopinga ukatili dhidi ya wanawake na mauaji nchini humo. Rais wa DRC Felix Tshisekedi alilihutubia taifa mbele y amabunge yote mawili, na kuonyesha kwamba Rwanda inatatiza usalama wa mashariki, siasa za Tanzania, Sudani, na Francois Bayrou ateuliwa kuwa waziri mkuu mpya wa Ufaransa pia hali nchini Israeli.

página 2 de 2